Zaburi 94:12-15
12
Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
13
unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
14
Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
15
Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
Settings