Skip to content
Zaburi 78:26-31

Zaburi 78:26-31

26
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options