Skip to content
Zaburi 78:23-28

Zaburi 78:23-28

23
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options