Zaburi 37:7-9
7
Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.
8
Epuka hasira na uache ghadhabu, usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.
9
Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.