Skip to content
Zaburi 25:1-7

Zaburi 25:1-7

1
Zaburi ya Daudi. Kwako wewe, Ee Bwana, nainua nafsi yangu,
2
ni wewe ninayekutumainia, Ee Mungu wangu. Usiniache niaibike, wala usiache adui zangu wakanishinda.
3
Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea atakayeaibishwa, bali wataaibishwa wafanyao hila bila sababu.
4
Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, nifundishe mapito yako,
5
niongoze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.
6
Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, kwa maana zimekuwepo tangu zamani.
7
Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala njia zangu za uasi, sawasawa na upendo wako unikumbuke, kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options