Zaburi 20:1-5
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki, jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2
Na akutumie msaada kutoka patakatifu na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3
Na azikumbuke dhabihu zako zote, na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4
Na akujalie haja ya moyo wako, na aifanikishe mipango yako yote.
5
Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. Bwana na akupe haja zako zote.
Settings