Zaburi 147:3-6
3
Anawaponya waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.
4
Huzihesabu nyota na huipa kila moja jina lake.
5
Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.
6
Bwana huwahifadhi wanyenyekevu lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.