Zaburi 119:27-30
27
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
28
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
29
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
30
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.