Zaburi 104:33-35
33
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.