Zaburi 102:13-17
13
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
14
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
17
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
Settings