Zaburi 10:7-11
7
Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.
8
Huvizia karibu na vijiji; kutoka mafichoni huwanasa wasio na hatia, akivizia wapitaji.
9
Huvizia kama simba aliye mawindoni; huvizia kumkamata mnyonge, huwakamata wanyonge na kuwaburuza katika wavu wake.
10
Mateka wake hupondwa, huzimia; wanaanguka katika nguvu zake.
11
Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau, huficha uso wake na haoni kabisa.”
Settings