Mithali 7:13-20
13
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
14
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
15
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
16
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
17
Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
18
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
19
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
20
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
Settings