Mithali 7:10-16
10
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
11
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
12
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
13
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
14
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
15
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
16
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
Settings