Skip to content
Mithali 4:20-27

Mithali 4:20-27

20
Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
21
Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
22
kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
23
Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24
Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
25
Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
26
Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
27
Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options