Mithali 1:28-31
28
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.