Skip to content
Hesabu 3:14-20

Hesabu 3:14-20

14
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options