Hesabu 10:14-16
14
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.