Mathayo 13:41-43
41
Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
42
Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43
Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
Settings