Marko 6:53-56
53
Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
54
Mara waliposhuka kutoka mashua yao, watu wakamtambua Yesu.
55
Wakaenda katika vijiji vyote upesi, wakawabeba wagonjwa kwenye mikeka ili kuwapeleka mahali popote waliposikia kuwa Yesu yupo.
56
Kila mahali Yesu alipokwenda, iwe vijijini, mijini au mashambani, watu waliwaweka wagonjwa wao masokoni. Wakamwomba awaruhusu hao wagonjwa waguse japo upindo wa vazi lake. Nao wote waliomgusa waliponywa.
Settings