Lumaktaw sa nilalaman
Luka 3:10-14

Luka 3:10-14

10
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
11
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
12
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
13
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
14
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options