Luka 24:44-45
44
Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
45
Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.