Luka 24:1-4
1
Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
2
Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
3
lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
4
Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.
Settings