Skip to content
Walawi 8:7

Walawi 8:7

Inaonyesha mstari 7 pamoja na muktadha unaouzunguka.
4
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
5
Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.”
6
Kisha Mose akamleta Aroni na wanawe mbele, akawaosha kwa maji.
7
Akamvika Aroni koti, akamfunga mshipi, akamvika joho na kumvalisha kisibau. Pia akafunga kisibau juu yake na kukifunga kiunoni mwake kwa mshipi wake uliosokotwa kwa ustadi.
8
Akaweka kifuko cha kifuani juu yake, na kuweka Urimu na Thumimu kwenye hicho kifuko.
9
Kisha akamvika Aroni kilemba kichwani pake, akaweka lile bamba la dhahabu, yaani ile taji takatifu, upande wa mbele wa kilemba, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
10
Ndipo Mose akachukua mafuta ya upako na kuipaka maskani na kila kitu kilichokuwamo ndani yake, kisha akaviweka wakfu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options