Walawi 8:3
Inaonyesha mstari 3 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Bwana akamwambia Mose,
2
“Waletee Aroni na wanawe mavazi yao, mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili na kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu.
3
Kisha kusanya mkutano wote kwenye ingilio la Hema la Kukutania.”
4
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
5
Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.”
6
Kisha Mose akamleta Aroni na wanawe mbele, akawaosha kwa maji.
Settings