Walawi 27:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Bwana akamwambia Mose,
2
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kama mtu yeyote ataweka nadhiri maalum ili kuweka watu wakfu kwa Bwana, kwa kutoa kiasi cha thamani inayolingana,
3
thamani ya kukomboa mwanaume mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na miaka sitini itakuwa shekeli hamsini za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu;
4
ikiwa ni mwanamke, weka thamani yake kwa shekeli thelathini.
Settings