Walawi 24:17-21
17
“ ‘Kama mtu yeyote atamuua mtu mwingine, ni lazima auawe.
18
Mtu yeyote auaye mnyama wa mtu mwingine lazima afidie, uhai kwa uhai.
19
Ikiwa mtu yeyote atamjeruhi jirani yake, chochote alichomtenda naye atatendewa:
20
iwapo amemvunja mfupa atavunjwa mfupa, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama alivyomjeruhi mwenzake, vivyo hivyo ndivyo atakavyojeruhiwa.
21
Yeyote auaye mnyama wa mtu lazima alipe fidia, lakini yeyote auaye mtu, lazima auawe.
Settings