Yoshua 10:16-18
16
Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
17
Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
18
akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.