Yohana 5:45-47
45
“Lakini msidhani kuwa mimi nitawashtaki mbele za Baba, mshtaki wenu ni Mose, ambaye mmemwekea tumaini lenu.
46
Kama mngelimwamini Mose, mngeliniamini na mimi kwa maana aliandika habari zangu.
47
Lakini ikiwa hamwamini aliyoandika Mose, mtaaminije ninayoyasema?”