Skip to content
Yohana 5:39-47

Yohana 5:39-47

39
Ninyi mnachunguza Maandiko mkidhani ya kuwa ndani yake mna uzima wa milele, maandiko haya ndiyo yanayonishuhudia Mimi.
40
Lakini mnakataa kuja kwangu ili mpate uzima.
41
“Mimi sitafuti kutukuzwa na wanadamu.
42
Lakini ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu.
43
Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, nanyi hamnipokei, lakini mtu mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea.
44
Ninyi mwawezaje kuamini ikiwa mnapeana utukufu ninyi kwa ninyi, lakini hamna bidii kupata utukufu utokao kwa Mungu?
45
“Lakini msidhani kuwa mimi nitawashtaki mbele za Baba, mshtaki wenu ni Mose, ambaye mmemwekea tumaini lenu.
46
Kama mngelimwamini Mose, mngeliniamini na mimi kwa maana aliandika habari zangu.
47
Lakini ikiwa hamwamini aliyoandika Mose, mtaaminije ninayoyasema?”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options