Yoeli 2:4-5
4
Wanaonekana kama farasi; wanakwenda mbio kama askari wapanda farasi.
5
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.