Ayubu 42:2-6
2
“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3
Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4
“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5
Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
6
Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
Settings