Yeremia 5:16-17
16
Podo zao ni kama kaburi lililo wazi, wote ni mashujaa hodari wa vita.
17
Watayaangamiza mazao yenu na chakula chenu, wataangamiza wana wenu na mabinti zenu; wataangamiza makundi yenu ya kondoo na ya ngʼombe, wataangamiza mizabibu yenu na mitini yenu. Kwa upanga wataangamiza miji yenye maboma mliyoitumainia.
Settings