Yeremia 14:11-12
11
Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
12
Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”