Isaya 3:18-23
18
Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,
19
vipuli, vikuku, shela,
20
vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,
21
pete zenye muhuri, pete za puani,
22
majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,
23
vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.
Settings