Isaya 26:1-6
1
Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji ulio na nguvu, Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.
2
Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lile lidumishalo imani.
3
Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye moyo wake ni thabiti kwa sababu anakutumaini wewe.
4
Mtumaini Bwana milele, kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.
5
Huwashusha wale wajikwezao, huushusha chini mji wenye kiburi, huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.
6
Miguu huukanyaga chini, miguu ya hao walioonewa, hatua za hao maskini.
Settings