Mwanzo 9:8-11
8
Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
9
“Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
10
pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
11
Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
Settings