Mwanzo 41:47-48
47
Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
48
Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.