Mwanzo 3:21
Inaonyesha mstari 21 pamoja na muktadha unaouzunguka.
18
Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.
19
Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako hadi utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo, kwa kuwa wewe u mavumbi na mavumbini wewe utarudi.”
20
Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.
21
Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
22
Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.”
23
Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa.
24
Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.
Settings