Mwanzo 1:1-3
1
Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
2
Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
3
Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.