Kutoka 30:17-19
17
Kisha Bwana akamwambia Mose,
18
“Tengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kwa ajili ya kunawia. Liweke kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, kisha uweke maji ndani yake.
19
Aroni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwa maji yatokayo katika hilo sinia.