Kutoka 30:1-5
1
“Tengeneza madhabahu kwa mbao za mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba.
2
Madhabahu hayo yawe mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zitakuwa kitu kimoja nayo.
3
Funika hayo madhabahu juu na pande zote na pia pembe zake kwa dhahabu safi, na uifanyizie ukingo wa dhahabu kuizunguka.
4
Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, ziwe mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko itumikayo kuibebea madhabahu.
5
Tengeneza mipiko kwa miti ya mshita na uifunike kwa dhahabu.
Settings