Mhubiri 3:1-4
1
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
2
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
3
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
4
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
Settings