Mhubiri 1:5-7
5
Jua huchomoza na jua huzama, nalo huharakisha kurudi mawioni.
6
Upepo huvuma kuelekea kusini na kugeukia kaskazini, hurudia mzunguko huo huo, daima ukirudia njia yake.
7
Mito yote hutiririka baharini, hata hivyo bahari kamwe haijai. Mahali mito inapotoka, huko hurudi tena.