Uasi wa Kuendelea Jangwani
22
Pia mlimkasirisha Bwana huko Tabera, Masa na Kibroth-Hataava.
23
Vilevile wakati Bwana alipowatuma kutoka Kadesh-Barnea, alisema, “Kweeni, mkaimiliki nchi ambayo nimewapa.” Lakini mliasi dhidi ya agizo la Bwana Mungu wenu. Hamkumtegemea wala kumtii.
24
Mmekuwa waasi dhidi ya Bwana tangu nilipowajua ninyi.
Settings