Kumbukumbu 6:15-19
15
kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
16
Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
17
Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
18
Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
19
kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
Settings