Kumbukumbu 6:11-19
11
nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,
12
jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
13
Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.
14
Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;
15
kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
16
Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
17
Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
18
Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
19
kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
Settings