Skip to content
Kumbukumbu 4:15-19

Kumbukumbu 4:15-19

15
Hamkuona umbo la aina yoyote siku ambayo Bwana alizungumza nanyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana,
16
ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lolote kama la mwanaume au mwanamke,
17
au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege yeyote arukaye angani,
18
au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki yeyote aliye ndani ya maji.
19
Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyo Bwana Mungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options