Kumbukumbu 28:38-42
38
Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.
39
Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.
40
Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.
41
Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.
42
Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.
Settings