Kumbukumbu 28:15-19
15
Hata hivyo, kama hutamtii Bwana Mungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:
16
Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.
17
Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.
18
Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ngʼombe na wana-kondoo wa makundi yako.
19
Utalaaniwa uingiapo na utokapo.
Settings