Skip to content
Kumbukumbu 14:3-20

Kumbukumbu 14:3-20

3
Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
4
Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
5
kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
6
Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
7
Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
8
Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
9
Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
10
Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
11
Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
12
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
13
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
14
kunguru wa aina yoyote,
15
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
16
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17
mwari, nderi, mnandi,
18
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
19
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
20
Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options